Bismillah
 

WELCOME TO

 
Muhammad

MADRASA AL-HIDAYA

Allah
 

MUSLIM SCHOOL OF RIGHT GUIDANCE

 

Al-Fatiha

Allah

Prophet Muhammad

Qur'an

Hadith

Home

What's New

Total Site Contents

Al-Fatiha

 

HADITHI ZA MTUME MUHAMMAD
(Amani iwe juu yake)

REHEMA NA UPOLE

1. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah (ر ) kuwa alisema, Mtume (ص ) amesema,   “Mungu alipoumba viumbe aliandika katika kitabu ambacho kiko kwake juu ya kiti chake cha enzi, kuwa huruma yangu inashinda hasira yangu”. (Bukhari na Muslim)

2. Imepokewa kutoka kwa Jarir Bin Abdallah (ر ) kuwa alisema, Mtume (ص ) amesema “Asiyewahurumia wenzake basi Mwenyezi Mungu naye hamhurumii”. (Bukhari na Muslim)

3. Imepokewa kutoka kwa Bi Aisha (ر ) kuwa alisema, Mtume (ص ) amesema, “Hakika Mwenyezi Mungu ni mpole na mwenye huruma, na anapenda upole na huruma. Na Mwenyezi Mungu humpa mtu kwa upole mambo ambayo hampi kwa kutumia nguvu, na Mwenyezi Mungu hampi mtu isipokuwa kwa upole.” (Muslim)

4. Imepokewa kutoka kwa Bin Abbas (ر ) kuwa Mtume (ص ) alimwambia Ashajj Abdilqais (ر ), “Una tabia (sifa) mbili ambazo Mungu anazipenda sana, nazo ni upole na uvumilivu”. (Muslim)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


HOME

DOOR 

WINDOWS