Bismillah
 

WELCOME TO

 
Muhammad

MADRASA AL-HIDAYA

Allah
 

MUSLIM SCHOOL OF RIGHT GUIDANCE

 

Al-Fatiha

Allah

Prophet Muhammad

Qur'an

Hadith

Home

What's New

Total Site Contents

Al-Fatiha

 

HADITHI ZA MTUME MUHAMMAD
(Amani iwe juu yake)

 

KURIDHIKA

1. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah ( ر ) kuwa alisema, Mtume ( ص ) amesema, “Mtazameni aliye katika hali ya chini kuliko nyinyi na wala msimtazame aliyewashinda kwa hali, na kufanya hivyo hamtopata kuidharau neema ya Mungu aliyewapa.” (Bukhari na Muslim)

2. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah ( ر ) kuwa alisema, Mtume ( ص ) alikuwa akimuomba Mungu akimwambia, “Ewe Mwenyezi Mungu, wape watu wa ukoo wa Muhammad kadiri ya mahitaji yao tu.” (Bukhari na Muslim)

3. Imepokewa kutoka kwa Anas Bin Malik ( ر ) kuwa alisema, “Mtume ( ص ) hakuwahi kabisa kula chakula mezani hadi kufa kwake, na wala kula mkate wa unga uliosagwa vizuri na kuchungwa, hadi kufa kwake.” (Bukhari)

4. Imepokewa kutoka kwa Abu Musa al-Ash‘ari ( ر ) kuwa amesema, “Bi Aisha ( ر ) alitutolea na kutuonesha shuka na kikoi kigumu. Kisha akasema, “Mtume ( ص ) alifia katika nguo hizi mbili.” (Bukhari na Muslim)

 

 

 

 

 

 

 


HOME

DOOR 

WINDOWS